Pata taarifa kuu
MAREKANI-UCHAGUZI-SIASA

Barack Obama amuunga mkono Biden kuwania katika uchaguzi wa urais Marekani

Aliyekuwa rais wa Marekani Barack Obama, ametangaza kumuunga mkono aliyekuwa Makamu wake Joe Biden kupeperusha bendera ya chama cha Democratic kumenyana na rais Donald Trump wakati wa Uchaguzi Mkuu mwezi Novemba.

Rais wa zamani wa Marekani Barack Obama, na makamo wake wa zamani Joe Biden (picha ya zamani).
Rais wa zamani wa Marekani Barack Obama, na makamo wake wa zamani Joe Biden (picha ya zamani). REUTERS/Jim Bourg
Matangazo ya kibiashara

Mpinzani mkuu wa Biden, Bernie Sanders alijondoa katika kinyanyanyiro cha kutafuta bendera ya chama hicho katika dakika za lala salama.

Jumanne wiki hii Makamu wa zamani wa rais wa Marekani Joe Biden, mgombea wa uchaguzi wa Novemba, alipokea rasmi uungwaji mkono kutoka kwa mpinzani wake mkuu katika chama cha Democratic, Bernie Sanders.

Hii ni hatua inampa nafasi ya moja kwa moja Joe Biden kuchuana dhidi ya rais Donald Trump anayemaliza muda wake katika uchaguzi wa Novemba mwaka huu.

Bernie Sanders, ambaye alisitisha kampeni yake ya kura za mchujo wiki iliyopita, alishiriki na Joe Biden katika hafla ya mtandao ambapo alitangaza kwamba janga la Covid lilipelekea kuepo na umoja ndani ya chama cha Democratic.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.