Pata taarifa kuu
CANADA-UCHAGUZI-SIASA

Chama cha Justin Trudeau chashinda uchaguzi Mkuu Canada

Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau ameshinda Uchaguzi Mkuu uliofanyika jana na kuongoza nchi hiyo kwa muhula wa pili, kwa mujibu wa matokeo ya awali.

Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau kulingana na ubashiri wa Uchaguzi Mkuu uliotolewa na vyombo vya habari Canada anaelekea kupata tena ushindi lakini hatakuwa na idadi kubwa mno ya viti bungeni.
Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau kulingana na ubashiri wa Uchaguzi Mkuu uliotolewa na vyombo vya habari Canada anaelekea kupata tena ushindi lakini hatakuwa na idadi kubwa mno ya viti bungeni. REUTERS/Stephane Mahe
Matangazo ya kibiashara

Televisheni ta Taifa CBC inabashiri kuwa, chama cha Liberal cha Waziri Mkuu Trudeau kinaelekea kupata ushindi, na hivyo kitaunda serikali, lakini hakitakuwa na idadi kubwa mno ya viti bungeni.

Tayari wafuasi wa chama hicho wameanza kusherehekea ushindi huo jijini Montreal, wakati huu wakisubiri hotunba kutoka kwa kiongozi wao.

Hata hivyo, wafuasi wa chama cha Conservative kinachoongozwa na Andrew Scheer ambaye ameleta ushindani mkubwa, wameonekana wenye huzuni, baada ya kubainika kuwa watapoteza katika Uchaguzi huu.

Mamilioni ya raia wa Canada walishiriki katika Uchaguzi huu, ulioshuhudia idadi kubwa ya wanawake wakiwania nyadhifa ya kuwa Waziri Mkuu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.