Pata taarifa kuu

Ukraine: Marubani watatu wa kivita wafariki baada ya ndege kugongana

Nchini Ukraine, marubani watatu walifariki wakati wa mafunzo siku ya Ijumaa. Pigo jipya kwa Kyiv, wakati nchi hiyo inaadhimisha Siku maksusi ya usafiri wa  anga Jumapili hii, Agosti 27.

Ndege aina ya Aero L-39 Albatros, iliyohusika katika ajali hiyo, ni ndege ya mafunzo. Hii ni ndege aina ya L-39 katika Grand Junction, Marekani tarehe 28 Mei 2015.
Ndege aina ya Aero L-39 Albatros, iliyohusika katika ajali hiyo, ni ndege ya mafunzo. Hii ni ndege aina ya L-39 katika Grand Junction, Marekani tarehe 28 Mei 2015. AP - Gretel Daugherty
Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu huko kyiv, Emmanuelle Chaze

Katika mkoa wa Zhytomyr, magharibi mwa Kiev, Jeshi la Anga limethibitisha vifo vya marubani wake watatu, waliofarikisik ya  Ijumaa Agosti 25 baada ya ndege za mafunzo za L-39 kugongana angani.

Mamlaka imetangaza kufunguliwa kwa uchunguzi kubaini sababu za mkasa huo uliotokea siku ya Ijumaa. Miongoni mwa wahanga rubani wa kivita aliyepewa jina la "Juice", ambaye alifanya mashambulizi kadhaa ndani ya gari lake aina ya Mig-29 kuhami, miongoni mwa mambo mengine, mji mkuu wa Kiev.

Kuwafunza marubani wake kwenye ndege aina ya  F-16

Vifo vya marubani hawa watatu ni pigo kwa Ukraine, ambayo inakuja katika wakati muhimu ambapo nchi iko katika mbio dhidi ya wakati kwa kutoa mafunzo, nchini Ukraine na nje ya nchi, vipengele vyake bora katika uongozaji wa ndege maarufu ya kivita ya F-16 iliyoahidiwa na washirika wake wa Magharibi. Serikali tayari imeonya kwamba ndege hizi zitawasilishwa mara tu marubani wake watakapofahamu matumizi yao, kwa upande wa Kyiv hii inamaanisha kuwa F16 hazitakuwa Ukraine hadi mapema 2024.

Aidha, watu wawili waliuawa na mmoja kujeruhiwa katika shambulio la bomu la Urusi katika kijiji cha Podoly cha Ukraine, karibu na mji wa Kupiansk, kaskazini-mashariki mwa nchi hiyo, alitangaza gavana wa eneo hilo Jumamosi Agosti 26.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.