Guinea: Rais wa zamani Alpha Condé aondoka Conakry na kuelekea Umoja wa Falme za Kiarabu
Kulingana na duru za kuaminika, ndege iliyombeba rais wa zamani wa Guinea, Gulfstream G-IV, imeondoka kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Ahmed Sekou Touré Jumatatu hii Januari 17, mapema alasiri.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Alpha Condé alipata ruhusa kutoka kwa Mamadi Doumbouya kuondoka nchini ili kupokea matibabu huko Abu Dhabi. Ameambatana na daktari wake, Dkt Kaba, na walinzi wawili.
Ndege yake, iliyoondoka Jumatatu Januari 17, 2022, inatarajiwa kuwasili Abu Dhabi. Mkuu huyo wa zamani wa nchi hapo awali alikuwa amepata idhini kutoka kwa mamlaka ya mpito kuondoka nchini kwa matibabu kwa muda wa mwezi mmoja.