Ushindi wa Sassou Nguesso waidhinishwa
Mahakama ya Katiba ya Congo- Brazaville imeidhinisha Jumanne wiki hii ushindi wa rais Denis Sassou Nguesso wa Machi 21, baada ya upinzani kupinga ushindui huo na kuwasilisha malalamiko yake mbele ya Mahakama ya Katiba.
Imechapishwa:
"Katika matokeo ya mwisho ya uchaguzi (...), Mahakama ya Katiba imefanya marekebisho muhimu. Mgombea urais Denis Sassou Nguesso anatangazwa mshindi baada ya kupata 88.40% ya kura ”, ameitangaza Auguste Iloki, rais wa mahakama ya juu zaidi nchini.
Wapinzani wa rais Nguesso walikataa kukubali matokeo hayo wakisema uchaguzi huo ulikumbwa na udanganyifu mkubwa.
Bwana Sassou-Nguesso alishinda kuidhinishwa kwa mabadiliko ya katiba mwaka jana ili kumruhusu agombee tena kwa muhula mwingine wa miaka 7 zaidi mamlakani.