Pata taarifa kuu
SUDANI-MAREKANI-USHIRIKIANO

Sudan yakaribisha tamko la Pompeo kuhusu kuiondoa katika orodha ya ugaidi

Serikali la Sudan imeridhia tamko la waziri wa mashauriano ya kigeni nchini Marekani, Mike Pompeo kuwa serikali ya Khartoum itaondolewa kwenye orodha ya mataifa yanayofadhili ugaidi.

Waziri Mkuu wa Sudan, Abdalla Hamdok wakati wa ziara yake jijini Darfur Novemba 4, 2019.
Waziri Mkuu wa Sudan, Abdalla Hamdok wakati wa ziara yake jijini Darfur Novemba 4, 2019. ASHRAF SHAZLY / AFP
Matangazo ya kibiashara

Pompeo kwa zaidi ya mara moja amesema Marekani inanuia kuondoa kikwazo hicho ambacho kimeathiri uwekezaji kwenye nchi ya Sudan, ingawaje mataifa hayo mawili bado yanaafikiana kuhusu fidia inayostahili kulipa wahanga wa shambulio la bomu la mwaka 1998.

Siku ya Alhamisi, Pompeo aliiambia kamati ya bunge la seneti kuhusu uhusiano wa kigeni kwamba sheria kuhusu fidia inapaswa kuwasilishwa mbele ya bunge hivi karibuni.

Uhusiano kati ya nchi hizo mbili ulikuwa umedorora kabisa kwa kipindi cha miaka 30 ya utawala wa Omar al-Bashir, aliyepinduliwa madarakani kufuatia maandamano makubwa.

Tangu mwaka 1993, wakati Rais Bashir alimpokea kiongozi wa mtandao wa al-Qaeda Osama bin Laden, Sudan iliwekwa kwenye orodha nyeusi ya "mataifa yanayounga mkono ugaidi".

Mwaka 1998, baada ya mashambulizi makubwa ya Al-Qaeda dhidi ya balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania, Washington iliendesha mashambuizi ya anga nchini Sudani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.