Pata taarifa kuu
Sudani-USALAMA-HAKI

Sudani: Miili 28 ya maafisa wa jeshi yagunduliwa Omdurman

Miili ya maafisa 28 wa jeshi la Sudan, waliohusika katika mapinduzi ya 1990 yaliyotibuliwa dhidi ya rais wa zamani wa nchi hiyo Omar al-Bashir, imegunduliwa kwenye kaburi la halaiki katika wilaya ya Omdurman, karibu na Khartoum amesema mwendesha mashtaka wa jamhuri.

Katika moja ya mitaa ya Omdurman, Juni 9, 2019.
Katika moja ya mitaa ya Omdurman, Juni 9, 2019. AFP
Matangazo ya kibiashara

Mapema wiki hii kesi mpya inayomkabili aliye kuwa rais wa Sudan Omar al-Bashir ilianza. Omar al-Bashir aliondoka madarakani baada ya mapinduzi ya kijeshi mwezi Aprili 2019.

Mapinduzi ya Omar El Bashir yalifanyika mwaka 1989 dhidi ya Sadiq al-Mahdi, Waziri Mkuu wa wakati huo wa Sudan na kushika hatamu za uongozi wa nchi.

Anatuhumiwa kukiuka agizo la katiba na anakabiliwa na adhabu ya kifo. Omar al-Bashir atahukumiwa na watu wengine 16, raia wa kawaida na askari, akiwemo Makamu wa Rais Taha na Jenerali Bakri Hassan Saleh.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.