Pata taarifa kuu
AFRIKA-MAWASILIANO-TANZANIA

Kongamano la wadau wa mawasiliano Afrika, kufanyika Tanzania Mei 25

Kongamano la wadau wa mawasiliano Afrika linatarajiwa kufanyika nchini Tanzania siku ya Ijumaa ya Mei 25 mwaka huu ambapo litawakutanisha wadau wa uhusiano na mawasiliano kutoka taasisi mbalimbali za ndani na nje ya Tanzania.

Rais wa Chama cha maofisa uhusiano Tanzania, PRST, Loth Makuza (kulia)akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mei 22, 2018
Rais wa Chama cha maofisa uhusiano Tanzania, PRST, Loth Makuza (kulia)akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mei 22, 2018 rfi/Fredrick Nwaka
Matangazo ya kibiashara

Kongamano hilo litafanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Ofisi ndogo ya Bunge la Tanzania iliyopo Dar es salaam kuanzia saa nne asubuhi hadi saa nane mchana.

Kongamano hilo lenye kichwa cha “Uchumi wa pamoja Afrika:Machango wa mawasiliano katika kuchochea ufanisi wa sera ya viwanda Tanzania na Afrika kwa ujumla”

Rais wa chama cha maofisa Uhusiano Tanzania, Loth Makuza ameiambia RFI Kiswahili kuwa kongamano hilo linafanyika ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya mawasiliano Afrika.

“Tukio hili linalenga wanataaluma katika nchi za Afrika kukutana na kujadili masuala mbalimbali na kutathimini mchango wa mawasiliano katika bara la Afrika,”.

Ripoti zaidi zinasema kwa mwaka huu, wiki ya mawasiliano inatazamiwa kuadhimishwa katika miji mikubwa 60 iliyopo Afrika, Asia na Ulaya.

 

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.