Boko Haram yaendelea na uharibifu wake Nigeria
Kundi la Boko Haram linaendelea na mashambulizi yake nchini Nigeria na katika nchi jirani. Kiongozi wa kundi hilo Abubakar Shekau ameapa kuendelea na mapambano yao ambayo ameyataja kuwa ya kitakatifu kwa Waislam.
Imechapishwa:
Hata hivyo baadhi ya viongozi wa dini ya Kiislam wametupilia mbali madai hayo na kutaja kuwa ni uzushi mtupu na kupaka matoke Uislam.
Kundi hili la wapiganaji lililowahi wateka wanafunzi wasichana zaidi ya 200 wa Chibok limefanya tena jaribio la kutaka kuwateka wanafunzi na walimu Kaskazini mwa Nigeria.
Kwa mujibu wa BBC vikosi vya jeshi la Nigeria vilishindwa hivi karibuni kumkamata kiongozi wa kundi la wapiganaji wa Boko Haram Abubakar Shekau katika operesheni maalum iliyofanyika.
Inaarifiwa kuwa baada ya siku nne kuielekea ngome ya Shekau kaskazini mashariki mwa Nigeria, wanajeshi hao waliamriwa kusitisha safari yao ya kusonga mbele.
Kwa mujibu wa vyanzo vya kijeshi vikosi vya Nigeria vinajipanga upya tayari kushambulia ngome kuu ya Shekau kwa minajiliya kumkamata hai.
Hata hivyo katika operesheni ya hivi karibuni, Shekau aliweza kutoroka jeshi lilipokaribia kufika eneo ambapo alikua, kwa mujibu wa chanzo hicho.
Serikali ya Nigeria wiki iliyopita imetangaza zawadi ya dola elfu nane kwa mtu atakatoa taarifa za kuwezesha kukamatwa Abukbakar Shekau, kiongozi Boko Haram.