Pata taarifa kuu
RSF-UHURU WA HABARI

RSF: Uhuru wa habari upo mashakani

Shirika la Kimataifa linalotetea wanahabari linasema, uhuru wa wahabari upo mashakani sana kote duniani, wakati ambapo wanahabari wengi wametoweka, na wengine wanafungwa katika nchi mbalimbali duniani.

Uturuki sasa ni jela kubwa duniani kwa waandishi wa habari pamoja na nchi kama vile China, Syria, Misri na Iran, , kwa mujibu wa RSF.
Uturuki sasa ni jela kubwa duniani kwa waandishi wa habari pamoja na nchi kama vile China, Syria, Misri na Iran, , kwa mujibu wa RSF. Paul Bradbury/Getty Images
Matangazo ya kibiashara

Reporters Without Borders, linasema wanahabari katika mataifa mbalimbali wanateswa, wanafungwa jela na hata kupotea katika mazingira yasiyoeleweka.

Barani Afrika baadhi ya mataifa yanayoelezwa kuongoza katika unyanyasaji wa wanahabari na uhuru wa kufanya kazi zao ni pamoja na DRC, Congo, Djibouti, Eritrea na Zimbabwe.

Hayo yanajiri wakati ambapo mapema wiki hii Mahakama ya kijeshi nchini Cameroon ilimhukumu kifungo cha maisha jela mwandishi wa habari wa Idhaa ya Hausa ya RFI nchini humo kwa kosa la kutetea ugaidi.

Hata hivyo uongozi wa RFI ulisema kuwa Ahmed Abba hana hatia yoyote, ukibaini kwamba alifanya kazi yake kulingana na sheria.
Uongozi wa RFI unaendelea kuomba Ahmed Abba achiwe huru mara moja.

RSF

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.