Iván Duque: Ninapanga kuliunganisha taifa letu lililogawanyika
Rais mpya wa Colombia Iván Duque, ambaye anatajwa kuwa mdogo zaidi kuwahi kutawala taifa hilo, amepiashwa na kuanza kuongoza taifa hilo la Amerika Kusini.
Imechapishwa:
Rais huyo mpya anamrithi rais aliyemaliza muda wake Juan Manuel Santos, baada ya kushinda Uchaguzi Mkuu mwezi Juni.
Akiwahotubia raia wa Colombia kwa mara ya kwanza akiwa rais , Duque ameahidi kuliunganisha taifa hilo na kuimarisha hali ya uchumi.
Aidha, Wakili huyo wa zamani ameahidi kupambana na ufisadi na wale wanaofanya makosa ya kuhujumu uchumi.
Pamoja na hayo yote, kiongozi mpya amewaambia raia wa nchi hiyo kuwa ana nia ya kuufanyia marekebisho mkataba wa amani uliofikiwa kati ya serikali iliyopita na waasi wa FARC.
Tangu mkataba huo mwaka 2016, FARC kimekuwa chama cha kisiasa na kinawakilishwa bungeni.
Rais wa zamni Santos amemtaka rais huyu mpya kuheshimu mkataba huo wa amani.