Pata taarifa kuu
AFCON 2019

Droo ya michuano ya AFCON 2019 yatangazwa

Shirikisho la soka barani Afrika CAF, limetangaza droo ya michuano ya kufuzu kucheza kombe la mataifa bingwa barani Afrika mwaka 2019 nchini Cameroon.

Droo ya michuano ya kufuzu mwaka 2019
Droo ya michuano ya kufuzu mwaka 2019 CAFonline
Matangazo ya kibiashara

Wenyeji wa michuano hii Cameroon, wamepangwa katika kundi moja la B na mabingwa mwaka 1976 Morocco, Malawi na Comoros au Mauritius.

Mabingwa mara saba Misri, watakutana na wapinzani wao wa Afrika Kaskazini Tunisia walioshinda taji hili mwaka 2004.

Nigeria itamenyana na mabingwa mwaka 1996 Afrika Kusini.

Kundi la G, nchi jirani Congo itamenyana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Michuano hii itaanza kuchezwa kati ya mwezi Machi na Novemba mwaka 2018, nyumbani na ugenini.

Droo kamili:
A: Senegal, Equatorial Guinea, Sudan, Sao Tome /Madagascar
B: Cameroon, Morocco, Malawi, Comoros/Mauritius
C: Mali, Gabon, Burundi, Djibouti/South Sudan
D: Algeria, Togo, Benin, The Gambia
E: Nigeria, South Africa, Libya, Seychelles
F: Ghana, Ethiopia, Sierra Leone, Kenya
G: DR Congo, Congo, Zimbabwe, Liberia
H: Ivory Coast, Guinea, Central African Republic, Rwanda
I: Burkina Faso, Angola, Botswana, Mauritania
J: Tunisia, Egypt, Niger, Swaziland
K: Zambia, Mozambique, Guinea-Bissau, Namibia
L: Cape Verde, Uganda, Tanzania, Lesotho

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.