Pata taarifa kuu
SOKA-UEFA

Cristiano Ronaldo aionya klabu yake ya Real Madrid licha ya kupata ushindi

Mshambuliaji wa klabu ya soka ya Real Madrid kutoka nchini Uhispania Cristiano Ronaldo, ameonya kuwa huenda timu yake ikaadhibiwa vikali katika siku zijazo ikiwa haitabadilika katika michuano inayoendelea ya  hatua ya makundi kuwania taji la klabu bingwa barani Ulaya UEFA.

Wachezaji wa klabu ya Sportin Lisbon na Christiano Ronaldo baada ya kufunga bao Septemba 14 2016
Wachezaji wa klabu ya Sportin Lisbon na Christiano Ronaldo baada ya kufunga bao Septemba 14 2016 Daily Telegram
Matangazo ya kibiashara

Kauli hii ya Ronaldo inakuja baada ya timu yake kuishinda Sporting Lisbon ya Ureno mabao 2-1 Jumatano usiku katika uwanja wao wa nyumbani wa Santiago Bernabeu.

Madrid ambao ni mabingwa watetezi wa taji hili, walijihakikishia ushindi katika dakika za lala salama  baada ya Alvaro Morata kutikisa nyavu dakika nne kabla ya kumalizika kwa mchuano huo.

Ronaldo ambaye aliwahi kuichezea Sporting Lisbon akiwa na miaka 12, alikataa kusherehekea goli alilofunga, na badala yake kuinua mikono yake kuonesha ishara ya kuomba radhi kwa mashabiki wa klabu yake ya zamani.

Matokeo mengine ya Jumatano usiku Septemba 14 2016:-

  • Manchester City 4-0 Borussia Monchengladbach
  • Bayer Leverkusen 2-2 CSKA Moskva
  • Tottenham Hotspur 1-2 Monaco
  • Real Madrid 2-1 Sporting CP
  • Legis Warszawa 0-6 Borussia Dortmund
  • Club Brugge 0-3 Leicester City
  • Porto 1-1 Kobenhavn
  • Olympique Lyonnais 3-0 Dinamp Zagreb
  • Juventus 0-0 Sevilla

Katika hatua nyingine, michuano ya hatua ya makundi kuwania taji la Europa League inaanza kutifua vumbi Alhamisi usiku.

Ratiba Septemba 15 2016:-

  • Nice vs Schalke 04
  • PAOK vs Fiorentina
  • Sporting Braga vs Gent
  • Southmptom vs Sparta Praha
  • Villarreal vs Zurich
  • Panathinaikos vs Ajax
  • Fayenoord vs Manchester United
  • Villarreal vs Zurich
Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.