Pata taarifa kuu
OLIMPIKI-BRAZIL 2016-RIADHA

Sumgong aweka historia kwa kuishindia Kenya medali ya dhahabu mbio za Marathon

Mwanariadha Jemima Sumgong kutoka nchini Kenya, ameishindia nchi yake medali ya kwanza ya dhahabu katika historia ya mbio za Marathon katika Michezo ya Olimpiki kwa upande wa wanawake.

Bingwa wa Mbio za Marathon kwa upande wa wanawake katika Michezo ya Olimpiki Jemima Sumgong
Bingwa wa Mbio za Marathon kwa upande wa wanawake katika Michezo ya Olimpiki Jemima Sumgong c.o0bg.com/rf
Matangazo ya kibiashara

Sumgong amemaliza mbio hizo kwa muda wa saa 2 dakika 24 na sekunde 04, akifuatwa na Eunice Jepkirui Kirwa raia wa Bahrain, ambaye alibadilisha uraia wake kutoka nchini Kenya mwaka 2013.

Bingwa wa dunia wa mbio hizi, Mwiethiopia Mare Dibaba, naye alimaliza wa tatu.

Jemima Sumgong akisherehekea ushindi nchini Brazil Jumapili Agosti 14 2016
Jemima Sumgong akisherehekea ushindi nchini Brazil Jumapili Agosti 14 2016 Daily Nation

Sumgong ataendelea kukumbukwa katika siku zijazo kwa kuwa Mkenya wa kwanza kupata medali ya dhahabu katika mbio hizi za Kilomita 42 katika michezo hii ya Olimpiki inayoendelea nchini Brazil.

Wakenya wengine kama Catherine Ndereba na Prisca Jeptoo, katika miaka iliyopita wamekuwa wakijaribu kupata medali ya dhahabu bila mafanikio.

Kuelekea katika michezo hii, Sumgong mwenye umri wa miaka 31, alishinda mashindano ya London Marathon mwezi Aprili mwaka huu.
 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.