DROGBA-CHELSEA-SOKA
Didier Drogba huenda akarudi kuichezea Chelsea
Mchezaji wa zamani wa klabu ya Chelsea Didier Drogba, anayechezea klabu ya Montreal nchini Canada anafikiria kurejea katika klabu yake ya zamani kuisaidia.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Uongozi wa klabu ya Montreal FC umethibitisha hamu ya Drogbar kurejea kuichezea Chelsea klabu ambayo ana uhusiano wa karibu lakini ukasisitiza kuwa bado inamuhitaji mchezaji huyo kutoka Côte d'Ivoire.
Drogba alikuwa uwanjani Jumamosi iliyopita wakati klabu yake Ya zamani ilipokuwa inacheza na Sunderland.
Drogbar aliicheza Chelsea kati ya mwaka 2004 na 2012 na kurejea tena mwaka 2014 na kuondoka mwaka huu baada ya kuisaidia klabu yake kunyakua ubingwa wa msimu uliopita.