Pata taarifa kuu
PAOLAND-SOKA

Bayern Munich: Robert Lewandowski aingia katika orodha ya watu waliovunja rekodi

Jumatatu wiki hii, mshambuliaji wa Bayern Munich Robert Lewandowski ameingia rasmi katika kitabu cha watu waliovunja rekodi kutokana na kufunga mabao matano dhidi Wolfsburg mwezi Septemba uliyopita, na kumpelekea kuvunja rekodi mara nne.

Robert Lewandowski (Bayern Munich) akisherehekeabao lake la tano dhidi ya Wolfsburg mjini Munich Septemba 22, 2015.
Robert Lewandowski (Bayern Munich) akisherehekeabao lake la tano dhidi ya Wolfsburg mjini Munich Septemba 22, 2015. Reuters/Michael Dalder
Matangazo ya kibiashara

Hivyo amepata rekodi ya mabao matatu kwa muda mfupi katika historia ya michuano ya Ujerumani(dakika 3 na sekunde 22). Sawa na mabao manne kwa muda wa (dakika 5 na sekunde 42) na vile vile mabao matano kwa muda wa (dakika 8 na sekunde 59). Pia amekua mchezaji wa kwanza katika historia ya Bundesliga kwa kufunga mabao matano baada ya kipindi cha kwanza cha mchezo kuanza akiwa kwenye benchi.

"Ilikuwa usiku wa kihistoria kwangu mimi", mshambuliaji wa kimataifa Poland, mwenye umri wa miaka 27, amesema, wakati akikabidhiwa vyeti vyake vinne. "Ilinichukua muda wa siku kadhaa kutambua, familia yangu ilipigwa na mshangao zaidi kuliko mimi", Robert Lewandowski ameongeza.

Lewandowski, ana mpango wa kutoa jozi ya viatu viliyompelekea kufunga mabao hayo 5 katika hali ya upendo. Tangu kuanza kwa msimu huu amefunga mabao 14.

Lionel Messi, Robert Lewandowski, Carlos Tevez na Cristiano Ronaldo (kutoka kushoto kwenda kulia).
Lionel Messi, Robert Lewandowski, Carlos Tevez na Cristiano Ronaldo (kutoka kushoto kwenda kulia). Reuters (montage RFI)

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.