Yanga yapata ushindi wa pili mfululizo
Ligi Kuu ya Tanzania bara iliendelea siku ya Jumatano huku mabingwa watetezi Yanga FC wakipata ushindi wa pili mfululizo.
Imechapishwa:
Wanajwagani hao wakicheza mchuano wake wa pili katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam waliwashinda Tanzania Prisons mabao 3 kwa 0.
Mabingwa wa zamani nao waliendeleza ushindi wao baada ya kuishinda JKT Mgambo mabao 2 kwa 0.
Maji Maji ilipata ushindi wa bao 1 kwa 0 dhidi ya Kagera Sugar, Mbeya City nao wakapata ushindi mkubwa wa mabao 3 kwa 0 dhidi ya Ruvu Stars.
Matoke mengine, Azam FC 2 Stand United 0, Mtibwa Sugar 2 Toto Africans 1, Ndanda 1 Coastal Union 0 na Mwadui 2 African Sports 0.
Michuano hiyo inaendelea siku ya Jumamosi:-
JKT Mgambo-Maji Maji
Stand United-African Sports
Tanzania Prisons-Mbeya City
Young Africans-Ruvu Stars
Jumapili:
Mwadui- Azam
Mtibwa Sugar- Ndanda
Simba- Kagera Sugar
Costal Union-Toto Africans.