Pata taarifa kuu

Kenya: Mahakama yatia breki mradi wa ujenzi wa nyumba za bei nafuu

Nairobi – Mahakama ya rufaa nchini Kenya, imeamua kuwa mpango wa utozwaji kodi unaotekelezwa na serikali ya rais William Ruto ili kujenga makaazi yenye bei nafuu, ni kinyume cha sheria.

Rais wa Kenya William Ruto alitia  saini muswada wa fedha 2023 kuwa sheria mwaka jana
Rais wa Kenya William Ruto alitia saini muswada wa fedha 2023 kuwa sheria mwaka jana © Statehouse Kenya
Matangazo ya kibiashara

Serikali ilikuwa imeiomba mahakama kuiruhusu kuendelea kutoza ushuru huo kutoka kwa mapato ya kila mwezi kutoka kwa raia walioajiriwa wakati ikisubiri kusikizwa kwa rufaa ya kupinga mpango huo wa utawala wa rais Ruto.

Mwezi Juni mwaka uliopita, Rais William Ruto alitia saini sheria ya fedha ya mwaka wa 2023, sheria ambayo imepingwa na baadhi ya raia na upinzani.

Serikali inasema mpango wake unalenga kuwajengea wakenya nyumba za bei nafuu.
Serikali inasema mpango wake unalenga kuwajengea wakenya nyumba za bei nafuu. © William Ruto

Kwa mujibu wa sheria hiyo raia wa taifa hilo la Afrika Mashariki wamekuwa wakikatwa asilimia 1.5, makato yanayolipwa kila mwezi na waajiri na wafanyikazi.

Mwezi Novemba,Mahakama ya Juu iliamua kwamba ushuru huo ulikuwa kinyume na katiba na kuizuia serikali kutekeleza mpango huo.

Utawala wa rais William Ruto unasema kuwa mpango huo unalenga kutoa ajira kwa vijana wengi ambao hawana ajira.
Utawala wa rais William Ruto unasema kuwa mpango huo unalenga kutoa ajira kwa vijana wengi ambao hawana ajira. © William Ruto

Serikali imetetea sheria hiyo ikisema kuwa inalenga kuwajengia raia wake wenye kipato cha chini nyumba za bei nafuu pamoja na kuunda nafasi za ajira.

Wakenya wamepata ahueni ya muda japokuwa  Mahakama ya Rufaa bado haijatoa uamuzi wake wa mwisho kuhusu sheria hiyo.

Baadhi ya raia wa Kenya wamekuwa wakipinga mpango huo wa serikali wakati wengine wakiuunga mkono.
Baadhi ya raia wa Kenya wamekuwa wakipinga mpango huo wa serikali wakati wengine wakiuunga mkono. © William Ruto

Uamuzi huo unakuja wiki moja baada ya mahakama ya rufaa kutoa idhini ya kutozwa ada ya bima ya afya yenye utata, ambayo itahitaji raia wa Kenya kuchangia  asilimia 2.75 ya mishahara yao ya kila mwezi kwa mpango wa afya ya kijamii.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.