Pata taarifa kuu

Kenya: Mahakama imetupilia mbali sheria kuhusu kodi ya makaazi

Mahakama nchini Kenya, imefuta sheria kuhusu kodi ya makaazi, ikisema ni kinyume cha Katiba, uamuzi ambao ni pigo kwa serikali ya rais Ruto ambayo kwa mujibu wake inajaribu kuliondoa taifa hilo kwenye changamoto za kiuchumi.

Rais wa Kenya William Ruto alitia saini muswada wa fedha 2023 kuwa sheria mwaka huu
Rais wa Kenya William Ruto alitia saini muswada wa fedha 2023 kuwa sheria mwaka huu © Statehouse Kenya
Matangazo ya kibiashara

Hatua hii imekuja baada ya serikali mwezi Juni, kuanza kuwakata wafanyakazi asilimia 1.5 ya mshahara wao kila mwezi ili kufadhili mpango wake wa ujenzi wa makaazi ya bei nafuu.

Aidha mwajiri pia amekuwa akimlipia mfanyakazi wake asilimia 1.5 ya mshahara, kufanikisha mpango huo

Jopo la majaji watatu wa mahakama kuu jijini Nairobi katika uamuzi wake limesema mpango huo haukufuata sheria kabla ya utekelezwaji wake ambapo pia haukuwajumuisha wafanyikazi katika sekta zote, suala ambalo wamelitaja kuwa la kibaguzi.

Rais Ruto ametetea mpango huo kuwa utasaidia kutengeneza ajira
Rais Ruto ametetea mpango huo kuwa utasaidia kutengeneza ajira © William Ruto

Kwa mujibu wa jaji wa mahakama hiyo, Jaji David Majanja, serikali kupitia mamlaka ya utozaji ushuru KRA, imezuiliwa kukusanya kodi hiyo ya makaazi.

Kodi hiyo ilikuwa sehemu ya sheria ya kifedha ya mwaka wa 2023, iliyoongeza ushuru kwa baadhi ya bidhaa, hali ambayo imeonekana kuwa mzigo kwa raia wa taifa hilo ambao tayari wanakabiliwa na mfuko wa bei za bidhaa.

Ghadhabu iliyotokana na hatua hiyo ya kupanda wa bei za bidhaa muhimu haswa chakula na mafuta, ilisababisha kutokea kwa maandamano dhidi ya utawala wa rais Ruto mapema mwaka huu.

Maandamano yalioongozwa na upinzani kupinga kupanda kwa gharama ya maisha yalishuhudiwa mapema mwaka jana.
Maandamano yalioongozwa na upinzani kupinga kupanda kwa gharama ya maisha yalishuhudiwa mapema mwaka jana. AP - Brian Inganga

Licha ya kukashifiwa, mkuu wa nchi ameteta mpango wa kutoza kodi ya makaazi kwa raia kwa madai kuwa utasaidia kuwajengea raia wake makazi bora pamoja na kutengeneza ajira na kupunguza ukopaji.

Wakosoaji wa rais Ruto wanamtuhumu kwa kwenda kinyume na kutozingatia ahadi alizozitoa kwa wapiga kura kuelekea uchaguzi mkuu wa mwezi Agosti mwaka wa 2022.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.