Gaza: Israel yashambulia Gaza wakati wa sikukuu ya Eid licha ya kukemewa na Marekani
Israeli imeshambulia eneo la Gaza leo, wakati waumini wa dini ya Kiislamu wakiadhimisha sherehe za Eid za kutamatika mfungo wa Ramadhan, shambulio linalojiri hata baada ya Marekani Kuonya Israel kuhusu mpango wake katika vita hivyo.
Imechapishwa:
Mamia ya Wapelestina waliojumuika kusherekea EID katika sehemu tofauti ikiwemo msikitu mkubwa wa Al-Aqsa,walielezea masikitiko yao kuwa walilazimika kusali wakati makazi yao yakiwa ni vifusi .
Walielezea tofauti na miaka ya nyuma ambapo walikusanyika katika msikiti huo, kusherekea ,walikutanyika, kutia moyo .
Israel imefanya mashambulio hayo ya ardhini na anga, siku moja baada ya waziri mkuu Benjamini Netanyahu kuapa kuwamaliza wapiganaji wa Hamas na kuwarudisha nyumbani mateka wa Israel.
Shambulio hili pia limetokea wakati mazungumzo ya Cairo kujaribu kutatuta mwafaka yakiongozwa na Misri, Qatar na Marekani, rais Biden akiwa amemwonya Netanyahu kuendelea kufanya kosa katika mbinu anazotumia katika mapigano hayo.