Pata taarifa kuu

Brics kuongeza uanachama wake hadi 11 mwaka ujao

Nairobi – Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ametangaza kuwa muungano wa BRICS utawasajili wanachama wapya sita mwanzoni mwa mwaka ujao.

Wachambuzi wa mambo ya kimataifa wanaona kuwa Brics inalenga kupata ushawishi na uungwaji mkono duniani kote
Wachambuzi wa mambo ya kimataifa wanaona kuwa Brics inalenga kupata ushawishi na uungwaji mkono duniani kote REUTERS - ALET PRETORIUS
Matangazo ya kibiashara

Iran, Argentina, Misir, Ethiopia, Saudi Arabia na Milki ya falme za kiarabu zitakuwa zinajiunga na muungano huo kuanzia tarehe moja ya mwezi Januari mwaka ujao kwa mujibu wa kiongozi huyo wa Afrika Kusini.

Mjadala wa kuhusu upanuzi wa muungano huo unaojumuisha nchi za Brazil, Urusi, India , China na Afrika kusini,  umetawala agenda ya kikao kilichofanyika jijini  Johannesburg.

Muungano huo umetangaza kuongeza wanachama wapya mwaka ujao
Muungano huo umetangaza kuongeza wanachama wapya mwaka ujao AFP - PHILL MAGAKOE

Kwa mujibu wa watu wa karibu na kikao hicho, hakujakuwa na tofauti zozote baina ya wanachama kuhusu upanuzi wa uanachama, mpango ambao umetajwa kuwa mwelekeo bora kutoka kwa mataifa wanachama.

Wachambuzi wa mambo ya kimataifa wanaona kuwa Brics inalenga kupata ushawishi na uungwaji mkono duniani kote.

Baadhi wanahisi kuwa muungano huo huenda ukawa ni mbadala wa ubabe wa mataifa ya Magharibi katika ulingo wa kimataifa
Baadhi wanahisi kuwa muungano huo huenda ukawa ni mbadala wa ubabe wa mataifa ya Magharibi katika ulingo wa kimataifa AFP - GIANLUIGI GUERCIA

Idadi kubwa ya mataifa yalikuwa yametuma maombi rasmi ya kujiunga na Brics, ambayo inawakilisha robo ya uchumi wa dunia na zaidi ya watu bilioni tatu.

Baadhi ya wakuu wengine 50 wa nchi na serikali wanahudhuria mkutano huo mjini Johannesburg, ambao unakamilika siku ya Alhamisi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.