Pata taarifa kuu

Vita nchini Ukraine: Utulivu warejea na hofu ya mashambulizi mapya ya Urusi yatanda Kyiv

Jumatatu hii, Oktoba 10, Moscow ilirusha makombora zaidi ya 80 katika mji mkuu wa Ukraine, Kyiv, lakini pia katika miji mingine mikubwa ya Ukraine, Ternopil, Dnipro, Lviv na Kharkiv.

Maafisa wasafisha mitaa ya Kyiv, saa chache baada ya mashambulizi ya Urusi kwenye mji mkuu wa Ukraine, Oktoba 10, 2022.
Maafisa wasafisha mitaa ya Kyiv, saa chache baada ya mashambulizi ya Urusi kwenye mji mkuu wa Ukraine, Oktoba 10, 2022. AFP - SERGEI SUPINSKY
Matangazo ya kibiashara

Takriban watu 19 waliuawa na mashambulizi hayo siku ya Jumatatu na 105 kujeruhiwa, kulingana na ripoti mpya iliyotangazwa Jumanne na mamlaka, katika mashambulizi haya ambayo pia yalilenga miundombinu ya nishati. Kwa upande wa mamlaka, wamesema Urusi inaweza kuendelea kushambulia mtambo wa umeme nchini Ukraine.

Katika kipindi cha saa chache kumeshuhudiwa mawimbi na mawimbi ya milipuko, sio yu hapa mjini Kiev, lakini pia katika maeneo mbali mbali ya nchi hii, kutoka Lviv magharibi mwa Kharkiv mashariki mwa ina Odesa katika kusini.

Ni vigumu kuelezea ni wapi kunalengwa, lakini taarifa kutoka katika wizara ya utamaduni ya Ukraine inasema majumba ya makumbusho na muziki yamepigwa kwa makombora.

Wakati huo huo, Jumanne asubuhi, jeshi la Urusi kwa mara nyingine tena lilishambulia mji wa Zaporizhia, ambapo maeneo ya makazi ya watu yalipigwa kwa bomu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.