Pata taarifa kuu

Joe Biden azungumza na Justin Trudeau na kutoa msaada dhidi ya moto nchini Canada

Rais wa Marekani Joe Biden ametoa msaada wake kwa Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau wakati wa mazungumzo ya simu kuhusu "moto mbaya na wa kihistoria" unaoikumba Canada, Ikulu ya White House imebaini leo Alhamisi, Juni 8, 2023. 

"Mioto hii hutokea mara kwa mara kwa sababu ya mabadiliko ya Tabia nchi," Justin Trudeau amesema kwenye Twitter.
"Mioto hii hutokea mara kwa mara kwa sababu ya mabadiliko ya Tabia nchi," Justin Trudeau amesema kwenye Twitter. ALEX DESJARALAIS via REUTERS - ALEX DESJARALAIS
Matangazo ya kibiashara

"Rais ameagiza timu yake kupeleka uwezo wote wa shirikisho wa kuzima moto ambao unaweza kusaidia haraka kuzima moto unaoathiri wananchi wa Canada na Marekani," White House imebaini katika taarifa, huku moshi kutoka kwa moto huo ukifunika sehemu kubwa ya kaskazini-mashariki mwa Marekani.

"Mamia ya maafisa wa kikosi cha Zima moto wa Marekani wamewasili hivi punde nchini Canada na wengine zaidi wako njiani," Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau alitangaza Jumatano jioni, baada ya kukutana na Rais wa Marekani Joe Biden.

"Mioto hii hutokea mara kwa mara kwa sababu ya mabadiliko ya Tabia nchi," Justin Trudeau amesema kwenye Twitter.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.