MAREKANI- SIASA
Vikao wa vya bunge nchini Marekani kuanza leo Jumanne
Kikao cha 118 cha bunge la wawakilishi nchini Marekani, kinafunguliwa hii leo, macho na masikio yakielezwa kwenye zoezi la kumchagua Spika mpya kuona iwapo mbunge wa Republican, Kevin McCarthy kutoka California anaweza kushinda nafasi hiyo.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Kushinda nafasi hiyo katika bunge hilo la wawakilishi 435-anapaswa kushinda kwa kura 218.
Uchaguzi wa katikati ya muhula uliofanyika mwezi Novemba mwaka uliopita, chama cha Republican ushindi mwembamba katika bunge hilo wa viti 222 dhidi ya 213 kutoka chama cha Democratic.
Spika anayemaliza muda wake Nancy Pelosi amekuwa kiongozi wa chama cha Democratic katika bunge hilo.