Pata taarifa kuu
MAREKANI-CHINA-USHIRIKIANO

Rais wa Marekani ampokea Xi Jinping

Ijumaa wiki hii, Rais wa Marekani Barack Obama amempokea Rais wa China Xi Jinping katika bustani ya Ikulu ya Marekani, nyimbo za mataifa hayo mawili zimepigwa, huku mizinga 21 ikirushwa hewani.

Rais wa Marekani Barack Obama na mwenzake wa China Xi Jinping Novemba 12, 2014 Beijing.
Rais wa Marekani Barack Obama na mwenzake wa China Xi Jinping Novemba 12, 2014 Beijing. MANDEL NGAN/AFP/Archives
Matangazo ya kibiashara

Ziara hiyo ya Xi Jinping nchini Marekani inatokea, huku kukiwa na mvutano kati ya mataifa haya mawili makubwa.

Ziara hii ya kwanza ya kiongozi wa China nchini Washington tangu kuchukua madaraka inakuja wakati ambapo uchumi wa China unaonyesha dalili halisi ya kudorora. Ziara hii ya Xi Jinping pia inakuja wakati Marekani imekua ikiilamu China kufanya udukuzi wa mawasiliano yake.

Serikali ya Marekani ina matumaini ya kuona ushirikiano kati ya China na Marekani "ukiimarika" katika suala la: mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi.

Kwa mujibu wa afisa wa Marekani, China inapaswa kutangaza Ijumaa wiki hii ikiwa ni pamoja na kuanzishwa mwaka 2017 kwa soko la kiwango cha gesi ya CO2 inayolenga kutoa bei ya mkaa ya mawe na hivyo kuhamasisha kupungua kwa uzalishaji wa gesi chafu katika sekta ya viwanda . Nchi inayozalisha kwa kiwango kikiubwa gesi chafu duniani tayari imefanya majaribio lakini bado haijaanzisha soko la kitaifa.

Katika mkutano wao mwezi Novemba mwaka 2014, mjini Beijing, Obama na Xi walitangaza mkataba ambapo waliwasilisha malengo yao katika suala la uzalishaji wa gesi chafu: kupunguza kutoka 26% hadi 28% ifikapo mwaka 2025 ikilinganishwa na mwaka 2005 kwa Umoja wa Mataifa, sawa na mwaka 2030 kwa China.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.