Pata taarifa kuu

Mkutano usio wa kawaida wa mawaziri wa ECOWAS kujadili migogoro katika kanda

Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) inafanya kikao kisicho cha kawaida cha baraza lake la upatanishi na usalama katika ngazi ya mawaziri Alhamisi hii mjini Abuja. Kwa mujibu wa ajenda, hali ya Senegal, pamoja na uamuzi wa Mali, Niger na Burkina Faso kujitoa katika jumuiya hii ya kikanda itakuwa mada kuu ya majadiliano.

Wakuu wa nchi wanachama wa ECOWAS mjini Abuja kwa mkutano wa kilele wa jumuiya ya kikanda, Desemba 10, 2023.
Wakuu wa nchi wanachama wa ECOWAS mjini Abuja kwa mkutano wa kilele wa jumuiya ya kikanda, Desemba 10, 2023. © KOLA SULAIMON / AFP
Matangazo ya kibiashara

 

Na mwandishi wetu wa kikanda, Serge Daniel

Kamishna wa Amani na Usalama wa Umoja wa Afrika (AU) anatarajiwa kushiriki katika mkutano huo Alhamisi hii mjini Abuja. Na msimamo wake uko wazi, anaelezea mwanadiplomasia: Jumuiya ya Kiuchumi ya Mataifa ya Afrika Magharibi (ECOWAS) na AU wanataka kuoanisha maoni yao kuhusu hali katika ukanda huo.

Mapendekezo yatatolewa kwa wakuu wa nchi wa taasisi ya kikanda wanaotarajiwa kukutana kuhusu masuala hayo mjini Addis Ababa kando ya mkutano ujao wa Umoja wa Afrika.

Kwa upande wa Senegal, lazima tuondoe ukungu haraka kutoka kwa maonyesho haya mazuri ya demokrasia ya bara la Afrika, anaeleza kwa uchache wa waziri anayeshiriki katika mkutano huo. Suluhu huko Dakar linaweza kuhusisha kuheshimu sheria na ukweli wa kisiasa wa eneo hilo, anabainisha mpatanishi mwingine.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari, ECOWAS imeitaka Senegal "kurejesha kalenda ya uchaguzi" lakini alipoulizwana France 24, Waziri wa Mambo ya Nje wa Senegal alikuwa wazi na alijibu kwamba Senegal ina ajenda yake.

"Senegal inaheshimu mapendekezo ya ECOWAS, lakini leo tunapendelea mantiki ya kisiasa ya ndani ambayo inaweza kusema kwamba kuahirishwa huku kwa uchaguzi ni fursa ya kuandaa uchaguzi huru, jumuishi na wa uwazi, " amesema Ismaila Madior Fall, Waziri wa Mambo ya Nje wa Senegal

Kujitoa ECOWAS

Mada nyingine kwenye jedwali la mkutano usio wa kawaida wa mawaziri wa Baraza la Usuluhishi na Usalama la ECOWAS, Mali, Niger na Burkina Faso. Nchi hizi tatu zinaendelea zimeapa kujitoa ECOWAS mara moja Zinajitoa katika ECOWAS bila kuheshimu tarehe ya mwisho ya kisheria ya mwaka mmoja. Hakuna hofu ndani ya jumuiya hii ya kikanda: "Tutapendekeza kwa wakuu wetu wa nchi kudumisha sera ya mikono iliyonyooshwa," anaamini mpatanishi mwingine. Kwa uthabiti zaidi, afisa wa tume ya ECOWAS anathibitisha kwa upande wake kwamba "ECOWAS sio kizuizi, lakini kuna masharti ambayo yanatakiwa kuzingatiwa kabla ya kujitoa".

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.