Pata taarifa kuu
SUDAN-MAZUNGUMZO

Umoja wa Mataifa wajaribu kusuluhisha pande zinazokinzana Sudan

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Volker Perthes amezindua mazungumzo yanayolenga kumaliza mvutano wa kisiasa nchini humo baada ya jeshi kuchukua madaraka na Waziri Mkuu Abdalla Hamdok kujiuzulu.

UMwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Volker Perthes akihutubia wanahabari mjini Khartoum Januari 10, 2022 na kutangaza kwamba Umoja wa Mataifa utaanzisha mazungumzo ya kuisaidia Sudan kutatua mzozo wake wa kisiasa unaozidi kuongezeka.
UMwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Volker Perthes akihutubia wanahabari mjini Khartoum Januari 10, 2022 na kutangaza kwamba Umoja wa Mataifa utaanzisha mazungumzo ya kuisaidia Sudan kutatua mzozo wake wa kisiasa unaozidi kuongezeka. ASHRAF SHAZLY AFP
Matangazo ya kibiashara

Mazungumzo hayo yanalenga kuwasaidia raia wa Sudan kujadiliana kuhusu kurejea kwenye njia ya demokrasia ili kumaliza mzozo unaoendelea.

Vuguvugu la Makundi mbalimbali ya kiraia yanayoshiriki kwenye maandamano yanayoendelea kushinikiza jeshi kuondoka madarakani, linasema halikufahamishwa kuhusu mpango  huo wa Umoja wa Mataifa.

Hata hivyo, msemaji wa vuguvugu hilo  Jaafar Hassan, amesema wapo tayari kushiriki kwenye mazungumzo hayo, iwapo yatalenga kuuundoa uongozi wa kijeshi na kurejeshwa kwa ule wa kiraia.

Muungano wa wasomi nao umekataa mpango huu wa Umoja wa Mataifa, ambao hata hivyo, umekaribishwa na mataifa ya Marekani, Uingereza, Falme za Kiarabu, Saudi Arabia na Misri.

Siku ya Jumatano, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, litakutana kujadili hali ya kisiasa na usalama nchini Sudan.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.