Pata taarifa kuu
SOMALIA-UCHAGUZI

Uchaguzi nchini Somalia kufanyika baada ya siku 60

Serikali ya Somalia imetangaza kuwa uchaguzi uliocheleweshwa sasa utafanyika ndani ya siku  60 zijazo, baada ya maelewano kati ya wanasiasa na wadau mbalimbali katika taifa hilo la pembe ya Afrika.

Rais wa Somalia Mohamed Abdullahi Mohamed,  anayefahamika pia kwa jina la Farmajo
Rais wa Somalia Mohamed Abdullahi Mohamed, anayefahamika pia kwa jina la Farmajo Yasuyoshi CHIBA / AFP
Matangazo ya kibiashara

Uamuzi huu umekuja baada ya kutamatishwa kwa mazungumzo ya kisiasa ambayo yamekuwa yakiendelea wiki hii mjini Mogadishu.

Waziri wa Habari Abdirahman Yusuf  ametangaza kuwa baada ya mashauriano hayo, imekubaliwa kuwa uchaguzi huo ufanyike ndani ya miezi miwili, na sasa tarehe kamili itatolewa na Tume ya Uchaguzi.

Waziri Mkuu Mohamed Hussein Roble amesema ni hatua ya kihistoria na pande zote zimekubaliana kuwa wajumbe maalum waliochaguliwa na wazee wa koo mbalimbali, watawachagua wabunge ambao, watamchagua rais.

Uchaguzi huu ulitarajiwa kufanyika mwezi Februari lakini serikali inayoongozwa na rais Mohamed Abdullahi Farmajo ikashinswa kuelewana na viongozi wa majimbo matano kuhusu namna ya kuufanikisha.

Hali hiyo ilizua sintofahamu ya kisiasa nchini humo na kufanya mambo kuwa mabaya ziadia baada ya wabunge kupitisha mswada wa kumwongeze muda wa miaka mliwili raius Farmajo, kitendo kilichoolaniwa na wanasiasa wa upinzani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.