Pata taarifa kuu
SOMALIA-UCHAGUZI

Mazungumzo ya siasa kuhusu Uchaguzi wa Somalia yaanza

Viongozi wa siasa nchini Somalia wameanza mazungumzo ya kupata mwafaka wa namna ya kuandaa uchaguzi uliocheleweshwa nchini humo.

Rais wa Somalia Mohamed Abdullahi Mohamed
Rais wa Somalia Mohamed Abdullahi Mohamed - AFP
Matangazo ya kibiashara

Mbali na wanasiasa nchini humo, mazungumzo haya yanawashirikishia pia wawakilishi kutoka Jumuiya ya Kimataifa.

Uchaguzi nchini Somalia ulikuwa umepangwa kufanyika mwezi Februari, lakini ikashindikana baada ya wanasiasa kushindwa kuelewana ni mfumo upi utumiwe kufanikisha uchaguzi huo.

Hali hiyo ilizua sintofahamu ya kisiasa nchini humo na kupelekea wabunge kumwongezea rais  Mohamed Abdullahi Mohamed, anayefahamika pia kwa jina la Farmajo, kuongoza kwa miaka miwili zaidi, hatua iliyoshutumiwa na wapinzani na jumuiya ya Kimataifa.

Mazungumzo yaliyoanza siku ya Jumamosi, yanaongozwa na Waziri Mkuu Mohamed Hussein Roble huku washirika wakuu wakiwa ni viongozi wa majimbo matano nchini humo.

Usalama umeimarishwa mjini Mogadishu, wanajeshi wa Umoja wa Afrika AMISOM wameonekana wakipiga doria, kuhakikisha kuwa mazungumzo hayo yanaendelea kwa usalama.

Haijafahamika ni lini mazungumzo haya yatamalizika na iwapo mwafaka utapatikana.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.