Ajali ya ndege yaua watu watano DRC
Watu watano wamepoteza maisha katika ajali ya ndege ndogo ya uchukuzi aina ya Antonov 2 ya shirika moja la ndege nchini humo. Ajali ambayo imetokea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia kwenye mpaka na Angola, kwa mujibu wa chanzo rasmi.
Imechapishwa:
Ndege hiyo ya shirika la ndege la Air Kasai ilianguka baada ya kuondoka kutoka mji wa Kamako, kusini mwa DRC wakati ambapo ingeliunganisha safari yake hadi Tshikapa, kilomita zaidi ya 150 kaskazini mwa DRC.
"Ndege ilianguka katika msitu, kilomita 3 kutoka Kamako baada ya kuondoka kuelekea Tshikapa. Watu wawili pekee, rubani na abiria mmoja, ndio wamenusurika, lakini hawajaongea mapaka sasa. Tuna idadi ya watu watano ambao wamepoteza maisha katika ajali hiyo, "amesema naibu mkuu wa eneo hilo, Anacletus Muswa Kapinga Safia.
Mnamo mwezi Juni ndege ndogo ya iliyokua ilikodiwa na shirika la Chakula Duniani (WFP) ilipata ajali ilipokua akipaa angani huko Kamonia na kusababisha watu kadhaa kujeruhiwa.