Pata taarifa kuu
UGANDA-SUDAN-KUSINI-USHIRIKIANO-USALAMA

Majeshi ya Uganda yaondoka Sudan Kusini

Kundi la kwanza la jeshi la Uganda linatarajiwa kuwasili nyumbani leo Jumatano likitokea nchini Sudan Kusini.

Majeshi ya Uganda yaanza kuondoka nchini Soudan Kusini, Jumatano Oktoba 21, 2015.
Majeshi ya Uganda yaanza kuondoka nchini Soudan Kusini, Jumatano Oktoba 21, 2015. AFP PHOTO/STRINGER
Matangazo ya kibiashara

Ripoti zinasema kuwa kundi hilo limekuwa likipiga kambi katika mji wa Bor Kilomita 190 Kaskazini mwa mji wa Juba.

Hatua hii inakuja katika utekelezwaji wa mkataba wa amani kumaliza machafuko nchini Sudan Kusini, ambao ulitaka wanajeshi wa Uganda kuondoka nchini humo.

Msemaji wa jeshi hilo la UPDF, Luteni Kanali Paddy Ankunda, amesema Sudan Kusini haitakuwa na sababu ya kutotekeleza mkataba huo wa amani baada ya jeshi la Uganda kuondoka kabisa nchini mwao.

Mapigano nchini Sudan Kusini yamesababisha vifo vya maefu ya watu, huku mamia kwa maelfu ya raia wakiyahama makaazi yao.

Machafuko nchini Sudani Kusini yalilipuka kufuatia ogomvi wa madaraka kati ya Rais Salva Kiir na aliye kuwa makamu wake Riek Machar, ambao wote ni kutoka makabila mawili tofauti.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.