Habari RFI-Ki
Umoja wa Mataifa umeiomba Burundi kushughulikia vurugu za kisiasa na kuheshimu haki za Binadamu
Imechapishwa:
Cheza - 10:07
Umoja wa Mataifa umetuma onyo kali kwa serikali ya Burundi na kuitaka kuchukua Hatua za haraka kushughulikia vurugu za kisiasa na kuheshimu haki za Binadamu.Aidha, Umoja huo umebainisha kwamba endapo vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu na uchochezi wa vurugu vitaendelea basi wahusika watawajibika mbele ya mahakama za kimataifa.Ungana Nami, Kupata maoni ya wasikilizaji wa Idhaa ya Kiswahili ya Radio France Internationale.