Urusi: Vladimir Putin aomba msaada wa Uturuki kusafirisha nje nafaka zake
Rais wa Urusi Vladimir Putin ameomba Jumatano hii, Agosti 2, 2023 kwa uungwaji mkono wa mwenzake wa Uturuki kuuza nje nafaka zake na kukwepa vikwazo vya Magharibi, huku akikataa kuzindua upya makubaliano ambayo, chini ya mwafaka wa Ankara, yaliwezesha mauzo ya nje ya kilimo ya Ukraine.
Imechapishwa:
"Kwa kuzingatia mahitaji ya chakula ya nchi zenye uhitaji zaidi, chaguzi zinatatuliwa ili kuwezesha usafirishaji wa nafaka za Urusi […].
Kuna nia ya kushirikiana katika eneo hili na Uturuki," Kremlin imesema katika taarifa, ikitoa maelezo kwa ufupi wa matamshi ya Bw.
Licha ya maombi ya mara kwa mara kutoka Uturuki na Umoja wa Mataifa, Urusi ilikataa mwezi Julai kurefusha mkataba huo ambao uliwezesha Ukraine kuuza nje nafaka zake kupitia Bahari Nyeusi, Kremlin ikizingatiwa kuwa masharti yaliyokusudiwa kuwezesha mauzo yake ya nafaka na mbolea hayajawahi kutekelezwa. Vladimir Putin alikariri kwa simu kwa Recep Tayyip Erdogan siku ya Jumatano kukataa kwake kuzindua upya makubaliano haya.