Pata taarifa kuu

Tetemeko la Ardhi: Uturuki yasitisha utafiti isipokuwa katika majimbo mawili

Uturuki imeamua siku ya Jumapili, siku kumi na nne baada ya tetemeko la ardhi la Februari 6, kusitisha zoezi la kutafuta miili isipokuwa katika majimbo mawili yaliyoathiriwa zaidi, Kahramanmaras na Hatay, imetangaza shirika la misaada la serikali (Afad).

Uturuki: katika kambi hii ya wanahewa huko Incirlik, Uturuki, ndege ya Antony Blinken imetua tu Februari 19, 2023. Ni kambi ya kimkakati kwa ajili ya kusafirisha misaada kwa waathiriwa wa tetemeko la ardhi.
Uturuki: katika kambi hii ya wanahewa huko Incirlik, Uturuki, ndege ya Antony Blinken imetua tu Februari 19, 2023. Ni kambi ya kimkakati kwa ajili ya kusafirisha misaada kwa waathiriwa wa tetemeko la ardhi. AP - CLODAGH KILCOYNE
Matangazo ya kibiashara

“Katika mikoa mingi juhudi za kutafuta miili limemalizika. Wanaendelea katika majimbo ya Kahramanmaras na Hatay, karibu na majengo arobaini”, ametangaza Unus Sezer, mkuu wa Afad.

Tetemeko la ardhi la kipimo cha 7.8 lililoharibu kusini mwa nchi hiyo na Syria liliua watu 40,689 nchini Uturuki, kulingana na ripoti rasmi ya hivi punde iliyotolewa na Afad siku ya Jumapili.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.