Gurudumu la Uchumi
Nchi za G20 zakubaliana kutoa fedha zaidi kusaidia kuinua uchumi wa dunia
Imechapishwa:
Cheza - 09:35
Mtangazaji wa makala hii juma hili ameangazia yale yaliyojiri kwenye mkutano wa wakuu wa nchi ishirini zilizoendelea kiviwanda duniani maarufu kama "G20", mkutano ambao uliwakutanisha wakuu hawa mjini Brisbane, Australia.Katika mkutano huu uliofanyika kuanzia tarehe 15 hadi 16 November mwaka huu, ulitoka na maazimio 22 ambayo yamelenga katika kufufua uchumi wa dunia na kutengeneza ajira zaidi kwa vijana.