Pata taarifa kuu

Mnigeria Asisat Oshoala achaguliwa kuwa mchezaji bora wa Afrika 2023

Mshambulizi wa Nigeria Asisat Oshoala, anayechezea FC Barcelona, alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa Afrika wa mwaka 2023 siku ya Jumatatu, wakati wa hafla iliyoandaliwa na Shirikisho la Soka la Afrika mjini Marrakech, Morocco.

Mchezaji nyota wa Nigeria Asisat Oshoala.
Mchezaji nyota wa Nigeria Asisat Oshoala. AFP - FRANCK FIFE
Matangazo ya kibiashara

Mfungaji nyota wa Super Falcons, Oshoala, 29, alikuwa mmoja wa watu muhimu katika uteuzi wa Nigeria ambao walifika hatua ya 16 katika Kombe la Dunia la FIFA msimu huu wa joto huko Oceania kabla ya kuondolewa na England.

Wakati wa mashindano haya, alikua mchezaji wa kwanza wa Kiafrika kufunga katika matoleo matatu ya Kombe la Dunia, akiwa tayari ameona nyavu mnamo 2015 na 2019.

Oshoala ameshinda mataji akiwa na Barca msimu huu, akishinda Champions League, ingawa walibanduliwa kwenye fainali dhidi ya Wolfsburg kutokana na jeraha, pamoja na Ubingwa na Kombe la Uhispania.

Alikuwa akiwania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika, pamoja na Thembi Kgatlana wa Afrika Kusini na Mzambia Barbara Banda.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.