Arsenal wamekamilisha usajili Declan Rice kutoka West Ham
Nairobi – Mchezaji wa kimataifa wa Uingereza Declan Rice amejiunga na Arsenal kutoka West Ham United kwa mkataba wa muda mrefu.
Imechapishwa:
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 24 tayari ana uzoefu mkubwa, akicheza mechi 245 akiwa na The Hammers na pia kushinda mechi 43 akiwa na Three Lions.
Declan alianza taaluma yake ya soka katika klabu ya Chelsea, kabla ya kujiunga na akademi ya West Ham mwaka 2014, na alisaini mkataba wake wa kwanza wa kitaaluma mwaka mmoja baadaye.
Katika siku ya mwisho ya msimu wa 2016/17, Declan mwenye umri wa miaka 18 alicheza mechi yake ya kwanza na hivi karibuni akawa sehemu muhimu ya kikosi chao cha kwanza kwa misimu sita iliyofuata.
A new chapter begins. pic.twitter.com/ha5Btd8I2h
— Arsenal (@Arsenal) July 15, 2023
Alitangazwa kuwa nahodha wa klabu hiyo mnamo Mei 2022 ambapo pia alishiriki katika michuano ya Euro 2020 na Kombe la Dunia la FIFA la 2022 akiwa na timu yake ya taifa ya Uingereza.
Mkurugenzi wa michezo katika klabu ya Arsenal, Edu, alisema Declan ni mchezaji mwenye tajiriba ya juu ambapo mchango wake utakuwa muhimu katika klabu hiyo ya Uingereza.
Arsenal's new #️⃣ 41! 🔴
— Sky Sports Premier League (@SkySportsPL) July 15, 2023
The moment Declan Rice was presented as a Gunner ⤵️ pic.twitter.com/L2mmF42xer
Meneja Mikel Arteta kwa upande wake ameeleza kuwa wamefurahia sana kwamba Declan anajiunga nao.