Nwankwo Kanu ateuliwa kuwa mwenyekiti wa klabu bingwa ya Nigeria
Mshambulizi wa zamani wa Arsenal na timu ya taifa ya Nigeria Nwankwo Kanu ameteuliwa kuwa rais wa klabu ya Enyimba, mabingwa watetezi na ngome ya kihistoria ya soka ya kitaifa, Gavana wa Mkoa wa Abia Alex Otti ametangaza.
Imechapishwa:
Kanu anamrithi Felix Anyansi-Agwu, kwenye usukani kwa miaka 24, ambaye chini ya utawala wake klabu hiyo, inayomilikiwa na serikali ya mkoa wa Abia (kusini), ilishinda idadi ya vikombe, ikiwa ni pamoja na Ligi ya Mabingwa Afrika mara mbili (2003, 2004).
Finidi George, mchezaji wa zamani wa Ajax na Betis na mchezaji mwenza wa Kanu katika timu ya Super Eagles, ndiye kocha wa sasa wa Enyimba, ambaye alishinda rekodi ya tisa ya ligi ya Nigeria mwezi Juni.