Pata taarifa kuu

Ombi la Dani Alves wa Brazil kuachiwa kwa dhamana limekatiliwa

NAIROBI – Kesi inayomkabili mlinzi wa timu ya taifa ya Brazil Dani Alves, imeendelea kuwa changamoto kwa upande wake baada ya Jaji wa mahakama mmoja nchini Uhispania kukataa ombi la pili la mchezaji huyo kupewa dhamana.

Daniel Alves mchezaji wa Brazil
Daniel Alves mchezaji wa Brazil AFP - ULISES RUIZ
Matangazo ya kibiashara

Haya yamejiri hapo jana siku ya jumanne tarehe 9 mwezi mei 2023 wakati  mwanasoka huyo akisubiri kusikilizwa kwa kesi yake ambayo anakabiliwa na  tuhuma za ubakaji.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 40 alizuiliwa mwezi Januari baada ya kushtakiwa kwa kumbaka msichana mdogo katika bafu la klabu ya usiku maarufu night clubs ya Barcelona mwishoni mwa mwaka jana.

Ombi la  Dani Alves la kutaka kuachiwa kwa dhamana limekataliwa na mahakama
Ombi la Dani Alves la kutaka kuachiwa kwa dhamana limekataliwa na mahakama AFP

Nyota huyo wa zamani wa Barcelona na Paris Saint-Germain atasalia rumande baada ya mahakama inayomchunguza kusema kuna "hatari kubwa" ya kujaribu kutoroka iwapo ataachiliwa kwa dhamana.

"Mahakama imekataa ombi la kuachiliwa lililotolewa na upande wa utetezi", Mahakama kuu ya haki ya Catalonia ilisema Jumanne utajiri wake "unaweza kumruhusu kuondoka Uhispania wakati wowote".

Hii ilikuwa ni mara ya pili kwa timu ya wanasheria wa Alves kushinikiza kuachiliwa kwake baada ya ombi lao la kwanza kukataliwa mnamo Februari.

Daniel Alves anakabiliwa na tuhuma za ubakaji
Daniel Alves anakabiliwa na tuhuma za ubakaji AP - Antonio Calanni

Mawakili wake waliomba dhamana tena mwezi Aprili mwaka huu, muda mfupi baada ya kufika mbele ya hakimu kwenye kikao cha pamoja ambapo walisema kuwa wawili hao walikuwa na mahusiano ya kimapenzi lakini wakadai kwamba walikubaliana.

Timu ya mawakili ya Alves ilipendekeza kubatilisha pasi zake mbili za kusafiria, za Brazil na Uhispania, ili kumhakikishia hakimu kwamba anaweza kupewa dhamana wakati huu - lakini ombi hilo lilikataliwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.