Pata taarifa kuu

Simba kuwasilisha malalamishi dhidi ya mashabiki wa Wydad kwa CAF

NAIROBI – Klabu ya Simba ya nchini Tanzania, inawazia  kuwasilisha kesi dhidi ya tabia za mashabiki wa klabu ya Wydad Athletic Club wakati huu wakijandaa kupambana katika mechi ya nduru ya pili katika michuano ya klabu bingwa barani Afrika. 

Wachezaji wa klabu ya Simba ya nchini Tanzania
Wachezaji wa klabu ya Simba ya nchini Tanzania © simba
Matangazo ya kibiashara

Hatua ya Simba inakuja  baada ya ushindi wao wa  goli moja bila ya jibu dhidi ya Wydad ambao ndio mabingwa watetezi wa ligi ya Mabingwa CAF.  

Rais wa CAF, Patrice Motsepe
Rais wa CAF, Patrice Motsepe © Pierre René-Worms

Kabla ya kuondoka nchini tanzania kuelekea Morocco, Simba itawasilisha rasmi malalamishi yao kwa Shirikisho la Soka barani Afrika CAF kufuatia matukio ambayo mashabiki wa Wydad waliyoyafanya kwenye uwanja wa Mkapa katika kipindi cha dakika10 za mwisho kabla ya kipindi cha kwanza kumalizika. 

Mashabiki wa  Wydad Athletic Club wanatuhumiwa kwa kuingia katika eneo la jukwaa moja la watu mashuhuri la VIP B bila ya kupewa kibali.

Kwa mujibu wa taarifa iliochapishwa na gazeti za Mwanaspoti nchini Tanzania, Mashabiki hao wamekuwa wakiambatana na timu hiyo kila mahali wanapokwenda na wanatajwa kuwa na vurugu kubwa kwenye mechi za ugenini kuliko nyumbani kwao. 

Mashabiki wa Simba ya nchini Tanzania
Mashabiki wa Simba ya nchini Tanzania © simba

Baada ya kuruka uzio huo wakati wa mechi hiyo,  waliwasha fataki za moshi ambao uliwazuia mashabiki wengine kuona pamoja na wachezaji na waamuzi kuona giza hali iliyomfanya mwamuzi kusimamisha mchezo. 

Msimu uliopita Simba iliwahi kukabiliwa na kasheshe la mashabiki kama hao wakipambana na  RS Berkane ya Morocco. 

Baada ya simba kuripoti wakati huo CAF iliwapa adhabu Berkane kwa kuwapunguzia idadi ya mashabiki kwenye mechi zao. 

Mechi ya simba dhidi ya Wydad Athletic Club
Mechi ya simba dhidi ya Wydad Athletic Club © simba

Baadhi ya video zilizosambaa katika mitandao ya kijamii ni sehemu ya ushahidi ambao maafisa wa klabu ya simba wamekusanya kama njia moja ya kujenga hoja katika kesi yao. 

Sio mara ya kwanza kwa mashabiki wa timu za kaskazini kuwasha vitochi katika uwanja hasa wakati timu zao zinakua hazifanyi vyema uwanjani. 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.