Mechi za robo fainali kuwania klabu bingwa barani Ulaya
NAIROBI – Mabingwa watetezi Real Madrid watacheza na Chelsea katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa huku Manchester City wakipangwa dhidi ya Bayern Munich katika droo iliyofanyika siku ya Ijuma.
Imechapishwa:
Viongozi wa Serie A Napoli watachuana na AC Milan katika mchuano utakaozikutanisha timu zote kutoka Italia wakati Inter Milan wakipangwa dhidi ya na vinara wa ligi ya Ureno Benfica.
Washindi wa mechi ya Real dhidi ya Chelsea watakutana na City au Bayern katika nusu-fainali.
Mechi za kwanza za robo-fainali zitachezwa Aprili 11 na 12, huku Real wakiwakaribisha Chelsea kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu kwanza kabla ya kusafiri London kwa marudiano wiki moja baadaye, na City wakiwa nyumbani kwa Bayern kwanza.
Inter walipangwa kucheza na Benfica nyumbani awali lakini sasa watasafiri hadi Lisbon kwa mechi ya kwanza ili kuepusha pambano kati ya AC Milan na Napoli huko San Siro.
Nusu fainali itachezwa mwezi Mei wakati fainali ikipangwa kupigwa mjini Istanbul ikipangwa Jumamosi, Juni 10.