Michuano ya soka kutafuta taji la wanawake yaendelea kushika kasi
Michuano ya soka kuwania taji la soka barani Afrika kwa upande wa wanawake, inaendelea wiki hii jijini Rabat nchini Morocco.
Imechapishwa:
Siku ya Jumatatu, kuna michuano ya kundi C ambako Nigeria itachuana na Afrika Kusini, huku Burundi nayo ikicheza na Botswana.
Matokeo ya kundi A:
Morocco 1-0 Burkina Faso
Senegal 2-0 Uganda
Kundi B:
Cameroon 0-0 Zambia
Tunisia 4-1 Togo
Ratiba ya Julai 4, 2022
Kundi C
Nigeria vs Afrika Kusini
Burundi vs Botswana
Wakati uo huo, Shirikisho la soka barani Afrika limetangaza kuongeza kiwango cha fedha anazôpata mshindi wa mashindano haya kwa asililia 150, kutoka Dola za Marekani kutoka 975, 000 hadi 2, 400 ,000
Mshindi wa kwanza atapokea Dola 500, 000, mshindi wa pili Dola 300, 000 na mshindi wa tatu Dola 200, 000.