Darwin Nunez ajiunga na kikosi cha Liverpool
Klabu ya Liverpool nchini Uingereza imemsajili mshambuliaji wa timu ya taifa ya Uruaguay Darwin Nunez, kutoka klabu ya Benfica nchini Ureno.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Darwin Nunez anajiunga na Liverpool kwa mkataba wa miaka sita na amesajiliwa kwa Pauni Milioni 64.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 anakuja katika klabu yake mpya akiwa na rekodi ya kuifungia Benfica mabao 34 katika mechi 41 alizocheza, msimu uliopita.