Argentina yaishinda Colombia kufuzu fainali ya Copa America
Emiliano Martinez, kipa wa timu ya taifa ya Argentina amekuwa shujaa, baada ya kuisaidia nchi yake kufuzu katika hatua ya fainali kuwania taji la soka, la Copa America huko Kusini mwa Afrika.
Imechapishwa:
Argentina imefuzu baada ya kuifunga Colombia mabao 3-2 kupitia mikwaju ya penalti, katika mchuano wa nusu fainali uliochezwa mjini Brasilia.
Lautaro Martinez aliipa Argertina bao la ufunguzi katika dakika ya 7 ya mchuano huo, kabla ya Luis Fernando Díaz Marulanda kuisawazishia Colombia katika dakika ya 61 ya mchuano huo.
Argentina sasa itachuana na Brazil katika mechi ya fainali ikayopigiwa siku ya Jumamosi katika uwanja wa Maracana jijini Rio de Janeiro.
Miaka miwili iliyopita, Brazil ilicheza na Argentina katika hatua ya nusu fainali na kushinda taji hilo.