UEFA-MICHEZO
UEFA kuamua kuhusu ushindi wa bao la ugenini
Uongozi wa Shirikisho la soka barani Ulaya, umetangaza kuwa kuanzia msimu ujao, bao la ugenini litafutwa katika mashindano ya Klabu bingwa, Europa League, na mashindano ya wanawake.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Tangu mwaka 1965, kanuni ya bao la ugenini imekuwa ikitumiwa, wakati timu mbili zinapocheza mechi mbili, nyumbani na ugenini na timu inayopata mabao mengi.
Mabadiliko hayo yanamaanisha kuwa, kuanzia msimu ujao, kutakuwa na muda wa ziada na mikwaju ya penalti, iwapo timu zote mvbili zitakuwa zimepata sare, ili kupata ushindi.