Michuano ya Euro hatimaye kuanza kutifua vumbi barani Ulaya
Michuano ya soka kuwania taji la bara Ulaya maarufu kama Euro 2020, iliyoahirishwa kutoka mwaka 2020 hadi mwaka 2021 inaanza siku ya Ijumaa nchini Uturuki.
Imechapishwa:
Mechi ya kwanza ni kati ya mabingwa wa zamani Italia na Uturuki, jijini Instanbul.
Kutokana na janga la Covid 19, mashabiki wanaotarajiwa kushuhudia michuano hii ni robô ya idadi ya kawaida.
Mabingwa watetezi Ureno, wamepangwa katika kundi moja na Hungary na mabingwa wa zamani Ufaransa na Ujerumani.
Mara ya mwisho kwa mashindano haya yanayofanyika kila baada ya miaka nne kufanyika ilikuwa ni mwaka 2016.
Muhimu
Mashindano haya yanaanza Ijumaa, Juni 11.
Michuano ya mwondoano itaanza Juni 26.
Fainali itachezwa Julai 11 katika uwanja wa Wembley, jijini London.
Mashindano haya yanafanyika wapi ?
Kwa mara ya kwanza, mashindano haya yanafanyika katika miji 11 ambayo ni London, Saint Petersburg, Baku, Munich, Rome, Amsterdam, Bucharest, Budapest, Copenhagen, Glasgow na Seville.
Timu ngapi zinashiriki
Kuna timu 24 zinazoshiriki, zimegawanywa katika makudni sita. Kutakuwa na mechi 51.
Kundi A: Uturuki, Italia, Wales, Switzerland
Kundi B: Denmark, Finland, Ubelgiji, Urusi
Kundi C: Uholanzi, Ukraine, Austria, Macedonia Kaskazini
Kundi D: Uingereza, Croatia, Scotland, Jamhuri ya Czech
Kundi E: Hispania, Sweden, Poland, Slovakia
Kundi F: Hungary, Ureno , Ufaransa, Ujerumani.
Mfumo wa mashindano
Timu mbili kutoka kila kundi, pamoja na timu nne bora zitakazokuwa zimemaliza katika nafasi bora za tatu, zitafuzu katika hatua ya robo fainali itakayokuwa na timu 16.
Mashabiki wataruhusiwa uwanjani ?
Ndio. Viwanja vyote 11 vimeruhusiwa kuwa na mashabiki.Shirikisho la soka barani Ulaya limeeleza kuwa viwanja kama Saint Petersburg na Baku, vitakuwa na asilimia 50 ya mashabiki.
Lakini viwanja vya Amsterdam, Bucharest, Copenhagen, Glasgow, Rome na Seville vikitarajiwa kuwa na kati ya asilimia 25 hadi 45 ya mashabiki.
London asilimia 25, Munich 22 na Budapest inatarajiwa kuwa na kairbu asilimia 100.