SOKA-SIMBASC-MTIBWA SUGAR
Simba yaishinda Mtibwa na kutwaa ngao ya hisani Tanzania
Msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2018/19 umefunguliwa rasmi hii leo kwa mchezo wa ngao ya hisani baina ya Simba na Mtibwa Sugar.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Mchezo huo umemalizika kwa Simba kupata ushindi wa mabao 2-1 ambayo yote yalifungwa kipindi cha kwanza cha mchezo.
Mabao ya Simba yalifungwa na Meddie Kagere na Hassan Dilunga wakati bao la kufutia machozi la Mtibwa lilifungwa na mshambuliaji Kelvin Sabato.
Hili ni taji la kwanza la Simba tangu ilipoanza kunolewa na Kocha Mbelgiji Patrick Aussems.