Ligi Kuu ya England kufikia tamati Mei 13
Ligi Kuu ya England inafikia tamati kesho Jumapili kwa mechi 10 kuchezwa kwa wakati mmoja.
Imechapishwa:
Liverpool ikiwa na alama 72 katika nafasi ya nne inahitaji alama moja ili kufuzu ligi ya mabingwa Ulaya wakati Chelsea inaomba Liverpool ishindwe ili yenyewe ishinde na kufuzu ligi ya mabingwa Ulaya.
Timu za Stoke City, West Bromwich na Swansea City zimeshashuka daraja.
Ratiba ya mechi za kesho ni kama ifuatavyo
Sauthampton inachuana na Manchester City
Swansea na Stoke City
Liverpool na Brighton and Hove Albion
Crystal Palace vs West Bromwich Albion
Burnley vs AFC Bournermouth
West Ham VS Everton
Newcastle vs Chelsea
Manchester vs Watford
Tottenham vs Leicester City
Huddesfierd Town vs Arsenal
Ligi hiyo pia inafikia tamati huku kiungo wa Manchester City Yaya Toure akitangaza kuondoka katika timu hiyo baada ya kuitumikia kwa misimu nane, akicheza zaidi ya mechi 200.