Pata taarifa kuu
CHAN 2018-UGANDA-SOKA

Kikosi cha mwisho cha Uganda chatajwa kuelekea fainali ya CHAN

Kocha wa timu ya taifa ya Uganda Mfaransa Sebastien Desabre amekitaja kikosi cha mwisho cha wachezaji 23, kinachojiandaa kushiriki katika fainali ya michuano ya CHAN kwa wachezaji wanaocheza soka nyumbani nchini Morocco siku ya Jumapili.

Kikosi cha timu ya taifa ya Uganda kinachoshiriki michuano ya CHAN 2018 nchini Morocco
Kikosi cha timu ya taifa ya Uganda kinachoshiriki michuano ya CHAN 2018 nchini Morocco www.fufa.co.ug
Matangazo ya kibiashara

Kikosi hiki cha mwisho kimekuja baada ya Uganda kupoteza mchuano wake wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Congo Brazaville mjini Rabat na kufungwa bao 1-0.

Wachezaji wawili waliochwa nje katika kikosi hicho Mustapha Kizza beki wa klabu ya KCCA na kiungo wa kati Tom Masiko kutoka klabu ya Vipers, wanarejea nyumbani jijini Kampala.

Kikosi kamili:

Makipa: Isma Watenga (Vipers Sc), Benjamin Ochan (KCCA FC), Saidi Keni (Proline FC)

Mabeki: Nico Wakiro Wadada (Vipers Sc), Joseph Nsubuga (Sc Villa Jogoo), Isaac Muleme (KCCA FC), Aggrey Madoi (Police FC), Timothy Dennis Awanyi (KCCA FC), Bernard Muwanga (Sc Villa Jogoo),  Mujuzi Mustapha (Proline FC).

Viungo wa Kati: Tadeo Lwanga (Vipers SC), Ibrahim Saddam Juma (KCCA FC), Muzamiru Mutyaba (KCCA FC), Milton Karisa (Vipers SC),  Abubaker Kasule (Express FC), Allan Kyambadde (SC Villa Jogoo), Paul Mucureezi (KCCA FC), Rahmat Senfuka (Police F.C).

Washambuliaji: Derrick Nsibambi (KCCA FC), Muhammad Shaban (KCCA FC), Nelson Senkatuka (Bright Stars FC).

Maafisa wa kiufundi:

Mkuu wa msafara: Hamid Juma (FUFA Mjumbe wa Kamati Kuu FUFA)

Kocha: Sebastien Desabre

Kocha msaidizi: Mathias Lule

Ratiba ya Uganda, (Kundi B)

  • Uganda v Zambia – Januari 14 2018 (Marrakech)
  • Uganda v Namibia – Januari 18 2018 (Marrakech)
  • Uganda v Ivory Coast – Januari 22 2018 (Marrakech)

Ratiba ya michuano ya ufunguzi:-

Kundi A: Morocco, Guinea, Sudan na Mauritania

  • Januari 13 2018:- Morocco v Mauritania
  • Januari 14 2018:-Guinea v Sudan

Kundi B: Ivory Coast, Zambia, Uganda na Namibia

  • Januari 14 2018:-Ivory Coast v Namibia
  • Januari 14 2018:-Zambia v Uganda

Kundi C: Libya, Nigeria, Rwanda na Equitorial Guinea

  • Januari 15 2018: Libya v Equitorial Guinea
  • Januari 15 2018: Nigeria v Rwanda

Kundi D: Angola, Cameroon, Congo na Burkina Faso

  • Januari 16 2018: Angola v Burkina Faso
  • Januari 16 2018: Cameroon v Congo
Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.