CAF-HAYATOU
Issa Hayatou azuru kenya
Rais wa Shirikisho la soka barani Afrika CAF Issa Hayatou anazuru jijini Nairobi nchini Kenya Alhamisi hii, wakati nchii ikijiandalia kuwa mwenyeji wa michuano ya CHAN 2018.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Isaa Hayatou ataongoza kikao cha Kamati ya Shirikisho hilo kuhusu maandalizi ya michuano ya mataifa bingwa barani Afrika kwa wachezaji wanaocheza soka nyumbani CHAN ya mwaka 2018.
Kenya inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Michuano hiyo ya bara Afrika baada ya Rwanda kuwa wenyeji mapema mwaka huu.
Wizara ya Michezo nchini Kenya imekuwa ikisema Kenya itakuwa tayari kuandaa michuano hii na ukarabati wa viwanja mbambali unaendelea.